.

.

.

.


TUMSIFU THE GREAT

BEHIND THE SCENE

  • MOVIE SHOOTING

    Wakati wa utengenezaji wa movie inayoitwa BACK TO SCHOOL
  • BACK TO SCHOOL

    SHOT IN TANGA TANZANIA
  • MUSIC VIDEO

    Wakati wa utengenezaji wa music video inakwenda kwa jina la I NEED U
  • MOVIE BACK TO SCHOOL

    Directed by TUMSIFU KOMBE
  • BACK TO SCHOOL

    wakati wa utrngenezaji wa movie inayoitwa BACK TO SCHOOL
  • MOVIE NAME-WIVU

    Behind the scene ya upigaji picha wa movie inayoitwa WIVU
  • MUSIC VIDEO HERE

    Upigaji wa picha wa Music video, msanii anajulikana kwa jina la Rider, wimbo DECEMBER, Shot in Tanga Tanzania
  • MOVIE-WIVU HERE

    Upigaji picha wa movie inayojulikana kwa jina la WIVU

Monday, October 22, 2012

ASKOFU,DR. STEPHEN MUNGA, ATOA RAI KWA WAKRISTO NCHINI


DR. STEPHEN MUNGA




Askofu  wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, ambaye pia ni Chancellor wa Sebastian Kolowa Memorial University{SEKOMU}  Dr. Stephen Munga awataka wakristo nchini kuwa na uvumilivu na kutokulipiza kisasi hasa katika kipindi hichi cha mgogoro baina ya wakristo na waislamu.
      Akiongea katika ibada ya kufungua mwaka wa 6 wa masomo katika chuo kikuu cha kumbukumbu ya Sebastian Kolowa,{SEKOMU} Mapema leo asubuhi tarehe 22 mwezi wa 10 chuoni hapo, aliwataka wakristo nchini kuwa wavumilivu na kutokulipiza kisasi kwa matukio ya uchomaji wa makanisa yaliyotokea hivi karibuni  huko mbagala Jijini Dar  es salaam tukio lililosababishwa na waumini wa dini ya kiislamu.
      Akitoa mifano kwa umakini mkubwa kutoka karne ya 3 na karne ya 4, Askofu Munga alisema ,
" KULITOKEA VITA VYA KUPINGA UKRISTO NA KUUFUTA KABISA, WALICHOMA BIBLIA ILI KUUMALIZA UKRISTO LAKINI UKRISTO MPAKA LEO UPO"
      Akiendelea kuwapa moyo wakristo Askofu Munga alisema 
" WANAWEZA KUCHOMA BIBLIA ZOTE, WANAWEZA WAKACHOMA MAKANISA YOTE, LAKINI HATUTATETEREKA KWA SABABU NENO LA MUNGU LIKO MIOYONI MWETU"
 Alionekana kusema maneno haya kwa uchungu huku akiukumbuka mchango na wosia wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
     Aidha Askofu Munga, alisisitiza swala la kutendeka kwa haki nchini kwa kuwataka viongozi wenye madaraka kuyatumia madaraka yao vema kwa manufaa ya jamii nzima na kusema matatizo yote lazima yatatuliwe kisheria huku akipinga  msemo wa 
 "AMANI HAIJI ILA KWA NCHA YA UPANGA"
 na kusisitiza kuwa majivu ya makanisa yaliyochomwa ni ishara ya kuzaliwa kwa Tanzania mpya yenye Amani ya kweli.

Pia aliwataka wanachuo wa chuo hicho wa dini zote kuwa wavumilivu na wenye kutenda haki kwa kuzingatia Imani za dini zao na Sheria za nchi, huku akitangaza siku ya Maombi kwa nhi nzima kwa Kumuomba Mungu kuiepushia Mbali Tanzania hili balaa la machafuko ya kidini

RIDER_DECEMBER OFFICIAL VIDEO, VIDEO DIRECTED BY TUMSIFU KOMBE THE GREAT

CHAZ MAVOKO-SONG KWAHERI, Video directed by Tumsifu the great films

wibiya widget

TUMSIFU THE GREAT © 2012.All Rights Reserved.Designed by Tumsifu Kombe Modified by Nicolaus Trac-0716 276 000 :ICT EXPERT Sponsored by: JIPANGE