EJIRO , mhitimu katika chuo kikuu cha Benin, afariki
dunia akiwa usingizini siku mbili kabla ya harusi yake katika mji wa Effurum
Nigeria. Ejiro pamoja na mchumba wake
ambaye ni daktari walikuwa wamepanga kuoana
na tayari walikuwa wameshatimiza taratibu zote za kimila. Ghafla siku ya
alhamisi jioni ikiwa ni siku mbili tuu kabla ya harusi yao binti huyo alianza
kulalamika kuumwa kichwa isivyo kawaida na kuanza kuongea maneno yasiyo ya
kawaida mithili ya mtu aliyechanganyikiwa
kitu kilichowashtua ndugu zake na kuamua kumkimbiza katika kanisa jirani
na kuombewa na mchungaji , baadaye usiku alifariki dunia akiwa usingizini.
CHANZO
CHA KIFO CHAKE.
Habari kutoka kwenye familia zinadai kutokuwa na
maelewano kati ya familia ya bibi na bwana harusi hao watarajiwa hasa kwa mama
wa bwana harusi aliyekuwa akiipinga ndoa ya mtoto wake huyo ambaye ni daktari
kumuoa binti huyo na kuitaka familia ya bibi harusi kuivunja ndoa hiyo haraka
iwezekanavyo.
Bwana harusi huyo siku za nyuma alionekana
kumlalamikia mama yake wazi wazi kwa kujaribu kumzuia kumuoa binti huyo, huku binti naye
akiapa kujiua endapo atazuiliwa kuoana mchumba wake huyo ambaye ni daktari. Siku
iliyofuata mama mkwe huyo alikiri kumuua mwali wake mtarajiwa huyo kwa uchawi
na kudai sababu ilikuwa hataki aolewe na mtoto wake kitu kilichowaacha ndugu na
majirani vinywa wazi.