.

.

.

.


TUMSIFU THE GREAT

BEHIND THE SCENE

  • MOVIE SHOOTING

    Wakati wa utengenezaji wa movie inayoitwa BACK TO SCHOOL
  • BACK TO SCHOOL

    SHOT IN TANGA TANZANIA
  • MUSIC VIDEO

    Wakati wa utengenezaji wa music video inakwenda kwa jina la I NEED U
  • MOVIE BACK TO SCHOOL

    Directed by TUMSIFU KOMBE
  • BACK TO SCHOOL

    wakati wa utrngenezaji wa movie inayoitwa BACK TO SCHOOL
  • MOVIE NAME-WIVU

    Behind the scene ya upigaji picha wa movie inayoitwa WIVU
  • MUSIC VIDEO HERE

    Upigaji wa picha wa Music video, msanii anajulikana kwa jina la Rider, wimbo DECEMBER, Shot in Tanga Tanzania
  • MOVIE-WIVU HERE

    Upigaji picha wa movie inayojulikana kwa jina la WIVU

Friday, November 8, 2013

PICHA :- TUKIO ZIMA LA KUKAMATWA KWA DAKTARI MSTAAFU AWAKITOA WANAWAKE MIMBA HUKO MOSHI

JESHI la polisi mkoani Kilimanjaro limefanikiwa kumnasa daktari mstaafu wa hospitali ya rufaa ya Mawenzi,mkoani Kilimanjaro, Frances Shayo(56) akiwa katika harakati za kuwatoa mimba wanawake wawili akiwemo Irene Musa(18) mwanafunzi wa shule ya sekondari Nkwereko iliyoko Masama wilayani Hai.

Daktari huyo ambaye anatajwa kufanya vitendo hivyo mara kwa mara amekamatwa pamoja na watu wengine watano wakiwa katika nyumba ya mkazi wa Kata ya Ng’ambo aliyefahamika kwa jina moja na Minde.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema daktari huyo amekuwa akifanya shughuli hiyo kwa muda mrefu katika eneo hilo na mara nyingine amekuwa akifanya shughuli za kuwatairi watoto katika nyumba ya rafiki yake huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari daktari Shayo amesema msichana huyo alifika katika nyumba hiyo akiwa na tatizo la kufunga kutokwa na damu hivyo alikuwa kwenye harakati za kutaka kumsaidia . 
 
Kwa upande wake mama mzazi wa binti huyo,Rozi Urasa amesema alifika nyumbani kwa daktari huyo baada ya kushauliwa na baadhi ya ndugu zake kumpeleka kutoa ujauzito huo kutokana na kwamba huenda binti huyo akakosa kazi pindi atakapokuwa akitafuta kazi akiwa na ujauzito

                                    PICHA KATIKA TUKIO HAPO CHINI

Askari polisi wakiwa na silaha wakiwa wamezingira nyumba iliyokuwa ikitumika kwa shughuli za kutolea Mimba


Daktari mstaafu wa hosptali ya rufaa ya Mawenzi Frances Shayo akiwa mikononi mwa polisi muda mfupi baada ya kumkamata akitaka kuwatoa mimba wasichana wawili.

Mmoja wa wanawake waliokutwa katika nyumba hiyo wakidaiwa kumsindikiza binti mmoja ambaye ni mwanafunzi kwenda kwa daktari huyo kutoa ujauzito.


Msichana Irene Musa ambaye anadaiwa kuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari Komkwa Masama wilayani Hai akitolewa kwenye nyumba ambayo anadaiwa kwenda kutolewa ujauzito .


Mmoja wa wanawake waliokutwa katika nyumba hiyo akidaiwa kwenda kutoa ujauzito kwa daktari huyo.

mati wa watu waliofika katika nyumba ambayo inadaiwa kufanyika vitendo vya kutoa mimba. Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.

RIDER_DECEMBER OFFICIAL VIDEO, VIDEO DIRECTED BY TUMSIFU KOMBE THE GREAT

CHAZ MAVOKO-SONG KWAHERI, Video directed by Tumsifu the great films

wibiya widget

TUMSIFU THE GREAT © 2012.All Rights Reserved.Designed by Tumsifu Kombe Modified by Nicolaus Trac-0716 276 000 :ICT EXPERT Sponsored by: JIPANGE