.

.

.

.


TUMSIFU THE GREAT

BEHIND THE SCENE

  • MOVIE SHOOTING

    Wakati wa utengenezaji wa movie inayoitwa BACK TO SCHOOL
  • BACK TO SCHOOL

    SHOT IN TANGA TANZANIA
  • MUSIC VIDEO

    Wakati wa utengenezaji wa music video inakwenda kwa jina la I NEED U
  • MOVIE BACK TO SCHOOL

    Directed by TUMSIFU KOMBE
  • BACK TO SCHOOL

    wakati wa utrngenezaji wa movie inayoitwa BACK TO SCHOOL
  • MOVIE NAME-WIVU

    Behind the scene ya upigaji picha wa movie inayoitwa WIVU
  • MUSIC VIDEO HERE

    Upigaji wa picha wa Music video, msanii anajulikana kwa jina la Rider, wimbo DECEMBER, Shot in Tanga Tanzania
  • MOVIE-WIVU HERE

    Upigaji picha wa movie inayojulikana kwa jina la WIVU

Thursday, April 12, 2012

TETEMEKO LA ARDHI LAUA ZAIDI YA 282 INDONESIA



 Zaidi ya watu 100 wameuawa na wengine wengi hawajulikani walipo kufwatia tsunami iliyosababishwa na tetemeko la ardhi katika pwani ya Sumatra nchini Indonesia.


 Maafisa wanaoshugulika na misaada pia wanajaribu kukabiliana na athari za mlipuko wa volkeno katika Mlima Merapi Katikati mwa Java.

Nyumba kadhaa ziliharibiwa na mawimbi ya bahari karibu na visiwa vya Mentawai.

Maji yaliyofurika yaliharibu kabisa vijiji kumi kwenye visiwa hivyo, afisa mmoja anayeshughulika na uokoaji aliambia shirika la habari la AFP.



walioachwa bila makao
Hali mbaya ya hewa na uharibifu imechelewesha juhudi za kufikia maeneo yaliyoathirika.

Hendri Dori Satoko,mjumbe katika visiwa vya Mentawai,aliambia kituo cha televisheni cha Metro: "takwimu zetu za hivi punde zinaonyesha kuwa watu 108 wameuawa na wengine 502 hawajulikani walipo."

Alisema baadhi ya wale ambapo hawajulikani walipo huenda walikimbilia maeneo salama ya juu na wanaogopa kurudi nyumbani kwao.

Maafisa wa wizara ya afya wanasema miili 113 imepatikana katika eneo hilo kufikia sasa,shirika la habari la Associated Press limeripoti.

Wakati huohuo maafisa wanasema zaidi ya watu elfu kumi na tatu wamehamishwa kutoka maeneo ya karibu na Mlima Merapi na kupelekwa katika kambi tangu mlipuko wa volkeno kutokea.

  
watu walioachwa bila makazi

Lakini hali imeelezewa kuwa ngumu kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotaka kuhama na kutafuta hifadhi katika maeneo salama.

Wakaazi wengi wa vijiji vilivyo karibu walipuuza onyo lililotolewa hapo awali na maafisa na hawakuwa tayari kuondoka na kuacha makao na mashamba yao.









TAARIFA Y HIVI PUNDE...

SHUGHULI ZA UOKOJI ZIKINDELEA
Vikosi vya uokoaji katika visiwa vya Mentawai wanasema mamia ya watu bado hawajulikani walipo,siku mbili baada tetemeko la ardhi kusababisha tsunami magharibi mwa Sumatra.


Maafisa wanasema kulikuwa na matatizo katika mtambo uliotengenezwa kwa lengo la kutoa tahadhari kwa wakaazi juu ya kuzidi kwa mawimbi.

Rais wa Indonesia amekatiza ziara yake ya nchini Vietnam ili aweze kutembelea visiwa hivyo pamoja na kusimamia shughuli za uokozi.

Rais Susilo Bambang Yudhoyono anatarajiwa kuzuru eneo hilo siku ya alhamisi kutathmini juhudi za misaada.

Pia ataelezwa kuhusu uokoaji katika eneo la Java, ambapo mlipuko wa volcano umesababisha maafa.

RIDER_DECEMBER OFFICIAL VIDEO, VIDEO DIRECTED BY TUMSIFU KOMBE THE GREAT

CHAZ MAVOKO-SONG KWAHERI, Video directed by Tumsifu the great films

wibiya widget

TUMSIFU THE GREAT © 2012.All Rights Reserved.Designed by Tumsifu Kombe Modified by Nicolaus Trac-0716 276 000 :ICT EXPERT Sponsored by: JIPANGE